Ukurasa wa nyumbani
 Uhamashishaji




Fasiri

Bahasa Indonesia
বাংলা / Baṅla
Català
中文 / Zhōngwén
English
Español
Filipino/Tagalog
Français
Galego
Ελληνικά / Elliniká
हिन्दी / hindī
Italiano
日本語 / Nihongo
Kiswahili
Polszczyzna
Português
Română
Русский
Српски / Srpski
Tiếng Việt
اردو / Urdu

                                        

Kurasa nyingine:

Visomo

Ramani ya tovuti

Maneno muhimu

Wasiliana nasi

Nyaraka za matumizi

Tovuti zinazohusiana

KUWA MHAMASHISHAJI

na Phil Bartle, PhD

imetafsiriwa na Wamalwa Philip


Kijitabu cha Mafunzo

Je umejiandaa kuwa mhamashishaji, mwelekezi au mwanaharakati?

Kujijaribu:

Kadiria ujuzi na maarifa uliyo nayo. Jiulize:
  • "Je nikotayari kupeana muda wangu na kuacha shughuli zangu ili kuwasaidia watu katika jamii kujitatulia matatizo yao wenyewe?"
  • "Je nina mienendo na tabia ambayo watu hawatanichukulia kama ambaye anajivuna?"
  • "Je ninaweza kufanya kazi katika jamii fulani bila kujiingiza kwenye siasa, migawanyiko na migogoro ilioko kwenye jamii hiyo?"
  • "Je ninaweza kudumisha matakwa na hamu ya watu wa jamii ninayoitumikia?"
  • "Je niko tayari kufanya kazi kwa namna ambayo watu wa jamii ninayoitumikia watahisi kuwa walijifanyia mambo wenyewe wala hawakufanyiwa?"
  • "Je nina ujuzi wa kutosha wa kimsingi katika mambo ya ukulima, teknolojia inayofaa, ujenzi, mambo ya ulemavu, ujenzi wa barabara, lishe, kazi ya jamii, kuhifadhi ardhi, usafi na maji; ili kuwasaidia watu katika jamii kutambua na kutatua shida zao wenyewe?"
  • "Je niko tayari kuepuka kuvujwa moyo wakati mambo yanapokwenda kinyume na nilivyotarajia au kukusudia?"
Ikiwa unavipaji hivi, basi utakuwa tayari zaidi kuwa mhamashishaji mwenye mafanikio.

Jukumu la Mhamashishaji:

Jukumu la mhamashishaji ni kuhamashisha jamii ili ikumbatie miradi itakayopelekea jamii hiyo kuongeza uwezo wake na kujitegemea.
Haswa, hiyo inajumulisha yafuatayo:
  • Kuita mikutano ya jamii ili:
    • kuwajulisha wanachama wa jamii yote juu ya habari sahihi kuhusu jinsi jamii hiyo inaweza kujitegemea; na
    • kuandaa na kutafuta rasilimali na vifaa vyote (vya kibinadamu na mali) vinavyohitajika kwa shughuli za miradi ya jamii;
  • Kusisimua watu katika jamii kushiriki katika miradi ya maendeleo ya jamii yao;
  • Kushiriki katika miradi ambayo itakuza ufanisi na uwezo wa jamii na kujitegemea;
  • Kuhakikisha kuwa habari zote ni sahihi na kwamba zimeeleweka vizuri;
  • Kukabiliana kwa dhati na habari za uwongo au sisizo sahihi, haswa zile zinazosababisha matarajio yasio na msingi au yaliopindukia, na ambayo hatimaye hufanya watu kuvunjika moyo;
  • Kuwatia moyo na kuwapongeza wana jamii, na kuwahakikishia kuwa wana uwezo wa kujiendeleza wenyewe;
  • Kuhakikisha kwamba maamuzi yote kuhusu miradi ambayo jamii itaanzisha ni chaguo la jamii yote na wala sio tu viongozi wa jamii wachache (wenye nguvu);
  • Kuhakikisha kwamba watu waliobaguliwa au wenye uwezo mdogo katika jamii wamesikizwa na kutiliwa maanani kwenye maamuzi ya jamii: wakiwemo wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, kabila la watu wachache, wanyonge na walionyimwa haki za uraia au ya kupiga kura;
  • Kuendeleza na kukuza umoja katika jamii, umoja wa nia maalum, umoja wa malengo na vitendo; na kukumbana kwa dhati na nguvu zinazochochea katika jamii migawanyiko, hisia za chuki, itikadi mbovu, ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa jinsia, ukabila, mapendeleo ya kiukoo na tabaka;
  • Kukutana mara kwa mara na wahamashishaji wengine ili kubadilishana ujuzi na uzoevu, kutatua matatizo yanayofanana pamaja na kuimarisha ujuzi wa kusisimua jamii na uongozi wa jamii.
  • Kuwasaidia viongozi na wanachama wa jamii kujifunza ujuzi na maarifa ya uongozi wa jamii.

Mhamashishaji wa jamii ni yule ambaye anasisimua jamii, na anatakiwa kuwa na maarifa na ujuzi kuhusu kanuni muhimu ya kuhamashisha jamii, na mwenye kiu ya kujifunza zaidi jinsi jamii zinaweza kusisimuliwa ili kuleta umoja na utangamano, kuzisaidia jamii kufanya maamuzi yake yenyewe, kujipangia miradi, kutambua na kutoa rasilimali yake kwa miradi hiyo, na kuchaguwa mikakati inayofaa zaidi kwa kutumia rasilimali za ndani na nje ili kufikia malengo ya jamii. Tazama: Majukumu ya Mhamashishaji.

––»«––

Mhamashishaji Kazini:


Mhamashishaji Kazini

© Hakimiliki 1967, 1987, 2007 Phil Bartle
Web Design: Lourdes Sada
––»«––
Imeratibishwa mwisho: 11.11.2011

 Nyumbani

 Uhamashishaji